Jose Mourinho amesema hana huruma na West Ham kwa sababu United wamekuwa wakifanyiwa maamuzi mabaya tangu mwanzo wa msimu
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesisitiza kuwa hana huruma na West Ham kufuatia ushindi wa 2-0 timu yake ilioupata katika uwanja wa London Jumatatu jioni.
Wagonga nyundo walimaliza mchezo vibaya kwa maamuzi mabovu ya mwamuzi Mike Riley, ambaye alimtoa kwa kadi nyekundu Sofiane Feghouli baada ya dakika 15 tu kabla ya Zlatan Ibrahimovic kufunga goli ambalo alikuwa ameotea.
Hata hivyo, Mourinho amelalama kuwa timu yake ilifanya makosa mengi ya maamuzi kwani hakuwa akifurahishwa na maamuzi ya waamuzi tangu mwanzo wa kampeni za msimu huu.
0 comments:
Post a Comment