Mtandao wa jana ulilipuka kwa post nzito baada ya Manchester United
kupoteza mchezo mwingine tena chini ya utawala wa Jose Mourinho.
Mashetani Wekundu hao wamefungwa mabao 2-1 dhidi ya Fenerbahce kwenye
Michuano ya Europa, na kuweka rehani mataumaini yao ya kufuzu hatua ya
mtoano.
Na kufuatia kipigo hicho ambacho ni cha tano kwenye michuano yote
msimu huu, baadhi ya mashabiki waliamua kumalizia hasira zao kwenye
mitandao ya kijamii na kutaka Mourinho afukuzwe na arejeshwe Sir Alex
Ferguson, ambaye alistaafu mwaka 2013
0 comments:
Post a Comment