Maelfu ya watu waliandamana usiku wa pili nchini Marekani kupinga ushindi wa mgombea wa chama cha Republican Donald Trump, ingawa hawakuwa wengi kama usiku wa kwanza.
Waandamanaji sana wamekuwa vijana ambao wanasema uongozi wa Trump utazua migawanyiko kwa misingi ya rangi na jinsia.
Hata hivyo, polisi eneo la Portland wamesema wamekabiliana na wezi na waporaji pamoja na watu wengine waliokuwa wanawashambulia wengine.
Akijibu maandamano hayo, Bw Trump ameandika kwenye Twitter kwamba "si ya haki".
Awali, alikutana na Rais Barack Obama ikulu ya White House na kumweleza kama mtu mzuri.
Hata hivyo, mwandishi wa BBC anasema licha yao kusema mkutano huo ulikuwa wa kufana, Bw Trump bado anaonekana kuwa tayari kubatilisha mambo mengi aliyoyafanya Obama alipokuwa madarakani. Miongoni mwa hayo ni Obamacare, sheria ya bima ya taifa iliyowawezesha Wamarekani wengi zaidi kuliko awali kupata bima ya matibabu.


0 comments:
Post a Comment