Alexis Sanchez amesema lipo jambo moja ambalo linamkera anapoambiwa na meneja wake alifanye kwenye kikosi cha Arsenal
Alexis Sanchez amesisitiza kuwa hali ya kikosi cha Arsenal miezi michache ijayo kitafahamu kama kinaweza kutwaa ubingwa Ligi Kuu msimu huu au la!
Washika Mtutu hao wa London wapo nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi pointi mbili nyuma ya vinara wa ligi Liverpool baada ya sare ya kukatisha tamaa ya 1-1 dhidi ya Tottenham Hotspurs wikiendi iliyopita.
Arsenal imekuwa na mwanzo mwingine mzuri lakini makosa ya mara zote mwisho wa kamepni katika miaka iliyopita humaanisha kikosi hicho cha Wenger hakipewi nafasi na yeyote kutwaa taji hilo.
Sanchezi ni aina ya wachezaji wanaopenda kufanya kazi kwa juhudi wanapokuwa dimbani na amesema kuwa hapendi Wenger anapomwambia apumzike.


0 comments:
Post a Comment