Mchezo huo unatarajiwa kuwa mgumu na wenye ushindani
wa aina yake kwani Mbao hawajapata ushindi kwenye mechi nne walizocheza
hivi karibuni
Pambano hilo limepangwa kupigwa uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza huo ukiwa ni mchezo wa tatu mfululizo baada ya kuzifunga Kagera Sugar, Toto African na kesho ni zamu ya Mbao.
Mchezo huo unatarajiwa kuwa mgumu na wenye ushindani wa aina yake kwani Mbao hawajapata ushindi kwenye mechi nne walizocheza hivi karibuni na mbaya zaidi wataingia kwenye mchezo huo wakitoka kufungwa mabao 2-0 na Kagera Sugar Jumatano iliyopita.
Kocha Ettiene Ndayiragije, amesema mchezo huo ni kama fainali kwao kuhakikisha wanarudisha mwendelezo wa kupata matokeo mazuri kama ilivyokuwa kwenye mechi walizocheza siku za nyuma
“Nafahamu Azam ni timu kubwa na nzuri lakini tumejipanga kufanya tunashinda mchezo huo ukizingatia tunacheza nyumbani mbele ya mshabiki wetu na kitu kingine kizuri tunataka kuwaonyesha mashabiki wetu kwamba kupoteza mechi zilizopita kulitokana na uchovu na siyo kuzidiwa,”amesema Ndaliyagije.


0 comments:
Post a Comment